USIZUNGUMZIE pesa zako mbele ya fukara na masikini.
Usizungumzie ubora wa
Afya yako mbele ya mgonjwa anayeteseka na magonjwa.
Usizungumzie nguvu
zako mbele ya Mnyonge tena ambaye unajua huna lengo la kumsaidia au pengine
nguvu zako ndio sababu ya mateso yake.
Usizungumzie furaha
yako mbele ya mwenye huzuni, vilio na majonzi.
Usizungumzie Uhuru
wako mbele ya mfungwa.
Usizungumzie
Mtoto/watoto wako mbele ya aliye tasa au mgumba au aliyefiwa na watoto wake.
Usizungumzie habari
za wazazi wako mbele ya walio mayatima.
Usizungumzie vyakula
na Vinywaji vyako mbele ya wanaolala na kushinda njaa.
Usiwazidishie
maumivu, maumivu unayowazidishia yaweza kukugharimu hata wewe.
Nisikilize, iko hivi;
Umepata kazi jifunze
kunyamaza!
Umepata mchumba
jifunze kunyamaza!
Umepata mtoto jifunze
kunyamza!
Umepitia hali ngumu
kiafya, kiuchumu au kimahusiano. Hebu nyamaza kimya!
Umepata mafanikio ya
kiuchumu au kimahusiano, hebu jifunze kunyamaza!
Umenunua kiwanja,
umenunua gari au nyumba kaa kimya.
Mwanao amefaulu au
wewe umefaulu kaa kimya.
Umevishwa pete ya
uchumba/umeoa/umeolewa, hebu jifunze kunyamaza!
Mahusiano yako yameyumba,
yamevunjika, mchumba kakukimbia? Ndoa iko arijojo inataka kuvunjika. Ndoa
imevunjika? Nyamaza kimya!
Unajiuliza Kwa nini
unyamze??
Wapo wengi wasiopenda
maendeleo yako! Wapo wengi wanatumia muda wao mwingi kukiharibu kile
ulichokipata! Kutangaza hatua ulizozipiga au changamoto unazopitia ni kuwapa
taarifa muhimu kuwa wao waanzie wapi kuviharibu zaidi. Kaa kimya fanya mambo
yako kwani siku zote Action speak louder than your words. Wacha maendeleo na
changamoto zako vizungumze. Never allow your enemies to trace your next move!
Roho za binadamu
zinapotoa maneno huwa yanajenga, kubomoa na hata kuumba kwa kuwa tunaamini kuwa
Mungu alituumba kwa sura na mfano wake na kumbuka Mungu aliumba kwa mdomo hivyo
basi midomo huumba maana ndani yetu imo pumzi ambayo ni Roho ya Mungu.
Roho za wanadamu
nyingi hazipendi wewe uendelee, hazipendi wewe uwazidi sasa iweje changamoto au
maendeleo kidogo tu tayari umekimbilia kuwatangazia kila kona ikiwemo Facebook,
Instagram, Twitter, Telegram, Tango n.k.
Unadhani wanafurahia
sana maendeleo yako? Unadhani hata ukielezea shida na changamoto za ndoa na
mahusiano yako mitandaoni watakuonea huruma na kukushauri lililo jema zaidi ya
kuchochea MOTO?

0 Response to "JIFUNZE KUNYAMAZA!"
Post a Comment